Yanga yatoa neno kuhusu sakata la Kabwili
Wednesday, January 29, 2020
Uongozi wa klabu ya Yanga umeibuka na kufunguka kuhusu sakata la tuhuma za upangaji matokeo zilizoibuliwa na mlinda mlango, Ramadhani Kabwili alipokuwa akiituhumu timu ya simba ambapo alidai kuaidiwa gari aina ya IST.
"Kilichofanywa hapa na Kabwili ni kuelezea historia ya tukio hilo kwa uzoefu wake kwenye kucheza mechi kubwa kama ile na umri wake ni mdogo pamoja na changamoto ambazo alikutana nazo", amesema Bumbuli.
"Kwahiyo kwa sababu suala limekuwa hivyo na sisi tumemuita mchezaji wetu tukae naye na atueleze kinagaubaga nini kimetokea, tukusanye ushahidi wote na tuupeleke kwenye vyombo vinavyohusika", ameongeza.
Mtazamo wa wengi unatofautiana kuhusu suala hilo, wapo wanaosema kuwa Kabwili amekosea kulisema suala hilo katika chombo cha habari na badala yake angelipeleka TFF tena mapema zaidi na wapo wanaosema yupo sahihi kwa kuwa masuala nyeti kama hayo hayapaswi kufumbiwa macho katika soka.


0Comments
Post a Comment