Back to Top

Maalim Seif kuchukua fomu ya kugombea nafasi ya uongozi katika chama cha ACT-Wazalendo

 Wednesday, January 29, 2020   

Chama cha ACT Wazalendo tayari kimetangaza rasmi kuanza kwa Uchaguzi wa Viongozi wa Kitaifa ndani ya Chama baada ya kukamilika chaguzi katika ngazi za chini. Shughuli ya kuchukua na kurejesha fomu kwa nafasi mbali mbali za uongozi katika ngazi ya Taifa imetangazwa kufanyika kuanzia tarehe 27 Januari hadi 26 Februari, 2020.

Kesho siku ya Alkhamis, tarehe 30/01/2020 saa 5.00 asubuhi, Maalim Seif Sharif Hamad anatarajia kuchukua fomu ya kugombea nafasi mojawapo kati ya nafasi za uongozi zilizotangazwa kugombewa katika Chama Cha ACT Wazalendo. Shughuli hiyo itafanyika Ofisi Ndogo ya Chama iliyopo Vuga, Zanzibar.

0Comments

Post a Comment